Ujumbe kutoka kwa Mkuu wa Chuo

Chuo Kikuu cha Kikristo  Elam (ECU) ni Taasisi ya Elimu ya Juu ya Mafunzo ya Kidini (Theolojia)  Chuo hiki kwa kifupi kinajulikana kwa jina la ECU  ambalo ni kifupi cha Elam Christian University.  Chuo hiki kinatoa mafunzo katika fani mbalimbali za kidini kwaajili ya kwatayarisha viongozi watumishi kwaajili ya mavuno ya nyakati za mwisho.

Chuo hiki kina usajili wa kimataifa kutoka katika  bodi ya Kimataifa YA Usajili wa Vyuo vya Biblia na Theolojia inayojulikana kwa jina la  the Association Independent Christian Colleges and Seminaries (AICCS) iliyoko Marekani. Kimesajiliwa kwa namba za usajili  219120M.   Vyeti vinavyotolewa na Chuo hiki vinatambuliwa kimataifa.Elam Christian University ni Taasisi isiyo ya kibiashara inayotoa mafunzo yenye ubora wa kitaifa na kimataifa katika kuwatayarisha viongozi watumishi.

 

ECU  inatoa mafunzo yasiyoegemea kwenye dhehebu lolote lile, bali mafunzo yenye msingi wa Ki-Biblia  yenye kuwatayarisha viongozi watumishi katika nyanja zote yaani kiroho, kimwili na kiakili  ili kuwezesha kila kiongozi mtumishi kutimiza kwa ufanisi  kusudi la wito wake. Mafunzo yanayotolewa katika chuo hiki ni nusu nadharia na nusu  vitendo, mwanafunzi anahimizwa kuyaweka katika vitendo yale ajifunzayo darasani.

 

Elam Christian University ni Chuo chenye wakufunzi na Wahadhiri mahiri ambao wamebobea katika kazi ya ufundishaji katika  elimu ya  Theolojia  na huduma.

Chuo hiki  ni cha Kipentekoste  na kinafanya kazi na madhehebu yote ya Kikristo yenye kukubaliana na maono yake. Chuo hiki pia kinapokea wanafunzi wa rangi, dini, jinsi  zote kutoka katika madhehebu na taasisi mbalimbali za kidini.  Pia chuo hiki kinapokea wanafunzi kutoka katika mataifa mbalimbali duniani na kuwatarisha katika maeneo ya huduma ili waweze  kuleta athali katika ulimwengu na kutimiza kusudi la wito wa kila mmoja wao.

 

Kwa niaba ya jumuiya ya Chuo Kikuu cha Kikristo Elam ninakukaribisha kwa moyo mkunjufu katika  chuo hiki  na ninafurahi kwamba unafikiria kujiunga nasi kwa masomo yako katika chuo  hiki. Chuo Kikuu cha Christian  Elam ni Chuo Kikuu cha Biblia, Theolojia  na Uongozi, kinachojulikana sana kwa viwango vya juu zaidi vya ufundishaji na ujifunzaji. Maono yetu ni kutambuliwa kama taasisi ya  Kidini  inayoongoza ulimwenguni kwaajili ya utayarishaji wa viongozi watumishi na Watendakazi waliokidhi vigezo vya kitaifa na kimataifa  katika kutumikia kusudi la Mungu duniani.

 

Chuo hiki kina kampasi na vituo vya mafunzo ndani na nje ya nchi. Chuo kina vituo vya mafunzo katika mikoa mbalimbali hapa Tanzania. Pia chuo hiki kina kampasi katika nchi za Malawi, Zambia, Kongo DR, Kenya. Pia chuo kinaendelea kufungua kampasi katika nchi mbalimbali duniani.

Chuo hiki kinatoa mafunzo kuanzia ngazi ya Atashahada (cheti) hadi ngazi ya Shahada ya Uzamivu (PhD) katika fani zifuatazo: Theolojia na Biblia, Theolojia na Huduma za Kanisa, Elimu ya Kikristo, Theolojia na Ushauri wa Kichungaji, Theolojia na Uongozi wa Kanisa, Kupanda Makanisa na Umisheni wa Ulimwengu, Uteteaji wa Imani ya Kikristo na  uamsho na mabadiriko ya Kiroho

Chuo hiki kimetayarisha mitaala ya mafunzoywenye kukidhi ubora wa kitaifa na kimataifa  unaoweka mkazo zaidi katika utendaji kuliko nadharia na unao mwandaa mwanafunzi katika maeneo au Nyanja zote ili kuleta ufanisi katika huduma.

 

Chuo hiki kinatoa mafunzo kwa  njia ya ana kwa ana  (darasani)  na kwa njia ya masafa. Kwa wanafunzi wanaosoma  kwa njia ya ana kwa ana wanafunzi huhudhuia mafunzo katika vituo vilivyoko katika mikoa na nchi mbalimbali. Kwa wanafunzi wanaosoma kwa njia ya masafa mafunzo hutolewa kwa njia ya mtandao na kwa njia ya posta. Wanafunzi wanaosoma kwa njia ya mtandao huhudhiria mafunzo kupitia madarasa ya mtandaoni yaani  mikutano ya zoom, watsapp na Telegram. Kila mwanafunzi huchagua mfumo wa kusoma kulingana na mazingira yake.

Mwongozo wa mafunzo ambao uko katika tovuti  hii utakuongoza kuchunguza masuala muhimu ya kitaaluma na kiutawala. Muhimu zaidi utakuongoza kupitia programu, muundo wa kozi na yaliyomo, wafanyakazi, na maelezo ya vifaa vya ustawi wa wanafunzi na pia kukuongoza kupitia michakato ya maombi na uandikishaji. Tunakuhimiza ujiunge nasi kwa masomo yako zaidi. Ikiwa kwa bahati yoyote kuna changamoto katika kutumia  Mwongozo wa Mafunzo (prospectus) tafadhali wasiliana nasi kwa ufafanuzi zaidi.

 

Napenda kutumia nafasi hii kukujulisha kwamba hujatembelea kwa bahati mbaya tovuti hii bali kwa kusudi takatifu la Mungu ili uweze kupata ufahamu kuhusu Elam Christian University na kisha ufanye aauzi ya kujiunga na chuo hiki

 

Napenda kukukaribisha kujiunga na mafunzo katika chuo chetu ili uweze kuandaliwa kaa kiongozi mtumishi katika kutumikia kusudi la Bwana wetu Yesu Kristo. Hakika hutabaki ulivyo baada ya kuhudhuria  mafunzo haya. Napenda kukuhakikishia kuwa hutajuta kusoma katika chuo hiki.

 

Ni mimi ndugu yako,

Rev.Prof. Erick L.Mponzi  (ThD)

MKUU WA CHUO

 

MAONO YETU

Chuo Kikuu cha Elam Christian kinalenga kuwa kitovu cha ubora wa kupata ujuzi wa kitaaluma kupitia
mafunzo, utafiti, ushauri, Huduma za Kanisa, na uinjilisti ulimwenguni kote ili kutimiza makuu
tume

DHAMIRA YETU

Chuo Kikuu cha Kikristo cha Elam kipo ili kutekeleza sehemu yake katika kutimiza masharti ya Utume mkuu wa Kristo kwa
kuelimisha watu katika kanuni za Maarifa ya Kikristo na kutoa elimu na mafunzo ya hali ya juu
kwa maisha ya Kikristo na Huduma. Kuwafunza mataifa na kuwafundisha kila kitu ambacho Kristo aliamuru
juu ya mitume wake (Mathayo 28:19)

MAADILI YETU YA MSINGI

Tunathamini mtaala wa kibiblia unaowaweka wanafunzi katika mafundisho sahihi ya kibiblia kupitia kitaaluma
ubora utakaowapa umuhimu katika ulimwengu wao, katika huduma ya utumishi wa Kikristo na katika maisha ya kila siku.Mapenzi kwa ajili ya kofia ya Mtumishi, Kipaumbele cha Kanisa, Kutafuta Mtazamo wa Kibiblia, Mazoezi ya Uadilifu na Uwakili.

FALSAFA YA ELIMU

Msingi wa mbinu za elimu za Chuo Kikuu cha Kikristo cha Elam ni kusadikisha kwamba Biblia ndiyo
Neno la Mungu na kwamba kufundisha neno la Mungu ndio msingi wa huduma ya Kikristo uangalifu mwingi unatolewa
kwa hiyo kwa masomo ya Biblia ambayo ni kitabu cha msingi cha maandishi na chanzo cha msingi.

Latest Articles

The latest articles from our blog, you can browse more

Our Partners

Long term partnerships with leading local and international companies

ELAM
ELAMCUEDU
Chuo KiKuu Cha Kikristo Elam
CHUO